Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 72 2016-02-02

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Je, Serikali itakamilisha lini ukarabati wa Mradi wa Maji wa Ntomoko ili kuwaondolea wananchi adha ya ukosefu wa maji kwenye vijiji vya Sambwa, Kirikima, Churuku, Jangalo, Jinjo, Hamai, Songolo na Madaha?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Selemani Nkamia, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ukarabati wa Mradi wa Maji wa Ntomoko ulianza kutekelezwa mwezi Februari, 2014 na mkataba wa kazi hii ulikuwa ni wa miezi sita. Kutokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha, kazi zilizopangwa kutekelezwa hazikuweza kukamilika katika kipindi cha miezi sita. Gharama ya mradi huo ni shilingi bilioni 2.87.
Utekelezaji wa mradi unaendelea na hadi sasa Mkandarasi amekwishalipwa jumla ya shilingi milioni 841.5 mwezi Agosti, 2015. Wizara ilituma shilingi milioni 600, mwezi Januari kwa ajili ya kuendelea na kazi. Aidha, Wizara itatuma shilingi milioni 728.7 mwezi Februari, 2016 na itaendelea kutuma fedha kwa ajili ya kukamilisha mradi huo. Wizara imejipanga kukamilisha mradi huo mwezi Aprili, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo utakapokamilika wananchi wa vijiji vya Makirinya, Hamai, Songolo, Kirikima, Lusangi, Madaha, Churuku, Jinjo, Kilele cha Ng‟ombe na Jangalo watanufaika na huduma ya maji.