Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 5 Sitting 1 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 08 2016-11-01

Name

Maida Hamad Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIDA HAMAD ABDALLAH aliuliza:-
Kwa kipindi kirefu suala la watumishi hewa limekuwa likiathiri sana uchumi wa Taifa na kwa kuwa waliohusika wengi wao ni maafisa na watumishi wa Serikali.
Je, Serikali inasema nini juu ya wale waliohusika kurudisha nyuma maendeleo ya nchi kwa njia hiyo?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maida Hamad Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia tarehe 25/10/2016 Serikali imechukua hatua za kinidhamu dhidi ya watumishi wa umma 1,663 kutoka katika Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambao walibainika kusababisha uwepo kwa watumishi hewa kwa mchanganuo ufuatao:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Wizara ni watumishi wa umma 16, kwa upande wa Idara zinazojitegemea na Wakala wa Serikali ni watumishi wa umma tisa, kwa Sekretarieti za Mikoa ni watumishi wa umma wa sita, Mamlaka za Serikali za Mitaa watumishi wa umma 1,632 inayofanya jumla ya watumishi 1,663.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua hii inajumuisha kuwasilishwa kwa masuala yanayohusu baadhi ya watumishi hawa katika vyombo vya ulinzi na usalama ambapo kufikia tarehe 25/10/2016 jumla ya watumishi wa umma 638 wamefunguliwa mashitaka polisi, watumishi 50 wanafanyiwa uchunguzi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na watumishi wa umma 975 mashtaka yao yamefikishwa kwenye mamlaka zao za kinidhamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hatua hizi Serikali inaendesha ukaguzi wa mara kwa mara kwa mfumo wa taarifa za kiutumishi au Human Capital Management Information System na maafisa wanaobainika kuhusika au kusababisha kuwepo kwa watumishi hewa katika taasisi au mamlaka zao wanachukuliwa hatua za kinidhamu kama vile kuwafungia dhamana na uwezo wa kuingia na kufanya kazi katika mfumo huo na hatua nyingine za kinidhamu. Nakushukuru.