Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 109 2016-09-16

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA (K.n.y. MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA) aliuliza:-
Sheria ya madini inawataka wachimbaji wakubwa kama vile GGM - Geita, kila miaka mitano wamege sehemu ya maeneo na kuyarudisha kwa wananchi.
(a) Je, ni lini Serikali itawarudishia wananchi maeneo ya Sami na Nyamatagata yaliyoombwa na wananchi kupitia vikao vyote hadi Mkoani?
(b) Je, ni lini eneo la STAMICO - Nyarugusu litafanywa kuwa la wachimbaji wadogo wadogo kama ambavyo Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alivyokwisha tamka mara mbili?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, lililoulizwa na Mheshimiwa Bukwimba Mbunge wa Geita Vijijini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya maeneo ya Sami pamoja na Nyamatagata yamo ndani ya leseni ya uchimbaji mkubwa wa madini ya dhahabu ya kampuni ya Geita Gold Mine (GGM) kupitia leseni namba SML 45/99. Hata hivyo Serikali inaendelea na mazungumzo na mgodi huo ili kampuni hiyo iweze kuachia baadhi ya maeneo yasiyohitajika kwa ajili ya kuwamilikisha wachimbaji wadogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la STAMICO na Nyarugusu lipo kitongoji za Buziba lina leseni ya utafutaji Na. PL 6545/2010 inayomilikiwa kwa ubia wa asilimia 45 na 55 kati ya STAMICO na kampuni ya TANZAM 2001, eseni hii itaisha muda wake tarehe 11 Julai 2018. Kwa kuwa eneo la Nyarugusu bado linamilikiwa na STAMICO pamoja na mbia wake ambapo Serikali pia ni mmiliki, Serikali inafanya mazungumzo na wamiliki hawa ili eneo hilo liachiwe sasa kwa ajili ya kumilikishwa wachimbaji wadogo wa eneo hilo.