Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 104 2016-09-16

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza:-
Baadhi ya watumishi wa DEPU mwaka 1999 – 2000 na Idara ya Uhamiaji hawajapandishwa vyeo mpaka sasa, licha ya kuwa na vigezo kama vya elimu na ngazi ya shahada huku wenzao wakiwa wamefikia vyeo vya Makamishna na Kamishna wasaidizi.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia watumishi kupata haki yao ya vyeo stahiki kama ilivyo kwa wenzao waliopandishwa vyeo?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi wa Idara ya Uhamiaji walioajiriwa mwaka 1999 – 2000 walikuwa na viwango tofauti vya elimu kama vile wengine wakiwemo kidato cha nne, wengine wa kidato cha sita, stashahada na wengine wakiwa na shahada. Katika watumishi wote hao hakuna aliyekuwa amefikia cheo cha Kamishna au Kamishana Msaidizi kama Mheshimiwa Mbunge alivyouliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, watumishi hao kwa sasa wametofautiana vyeo kutokana na sababu zifuatazo:-
Moja, waliajiriwa katika vyeo tofauti kulingana na elimu zao wakati wanaajiriwa na kujiunga katika mafunzo ya awali ya uhamiaji.
La pili; baadhi yao walijiendeleza kielimu wakati wapo katika ajira ili kuinua viwango vyao vya elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuchukuliwa hatua za kinidhamu na kisheria na kupelekea wengine kusimamishwa kupata vyeo kama ambavyo iko kwenye Sheria za Utumishi wa Taasisi hii.