Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 103 2016-09-16

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA I. ALEX aliuliza:-
Kumekuwa na uuzaji holela wa vifaa hatarishi barabarani kama vile visu, mapanga na kadhalika.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha biashara hii ambayo ni hatari kwa usalama wa wananchi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kumekuwa na uuzaji holela wa vifaa hatarishi barabarani. Vifaa hivi hutumika kwa shughuli mbalimbali kama vile kilimo. Hata hivyo vinaweza kutumika vibaya na kuhatarisha maisha ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe ushauri kwa Halmashauri zetu zote na mamlaka zinazohusiana na biashara kutenga maeneo maalum na kusimamia vema biashara hizo. Aidha, kama hali hii itaendelea Serikali haitasita kuchukua hatua stahiki kukomesha biashara ambayo inaweza ikaleta hatarishi pindi itakapotumika vibaya.