Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 69 2016-09-13

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-
Sudan Kusini imekubaliwa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Je, ni lini Serikali itafungua Ubalozi katika nchi hiyo ili kutengeneza mazingira ya kunufaika na fursa zilizoko katika nchi hiyo?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Taifa la Sudan Kusini lilianzishwa mwezi Julai, 2011 baada ya kura za maoni za wananchi wa nchi hiyo kuamua kujitenga kutoka nchi ya Sudan na kuunda Taifa jipya ya Sudan Kusini. Aidha, mwezi Aprili, 2016 nchi ya Sudan Kusini ilijiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kwa sasa Tanzania haina Ofisi za Ubalozi nchini Sudan Kusini. Katika kipindi hiki ambacho Serikali haijafungua Ubalozi nchini Sudan Kusini, shughuli za Kibalozi kwa nchi hiyo zinafanywa na Ubalozi wetu, Nairobi nchini Kenya.
Malengo ya Wizara kwa mwaka 2016/2017 ni pamoja na kuongeza uwakilishi wetu nje ya nchi kwa kufungua Balozi mpya na Ofisi za Kikonseli hususan katika nchi ambazo Taifa linanufaika zaidi na fursa za kiuchumi kama vile soko la bidhaa zetu, biashara, uwekezaji, ajira pamoja na utalii.
Aidha, naomba ieleweke kuwa licha ya kuwepo kwa fursa hizo, maamuzi ya kufungua Ofisi za Ubalozi nchini Sudan Kusini pamoja na uendeshaji wa shughuli za Ofisi za Ubalozi zitakazofunguliwa zitategemea na Serikali itakapokuwa tayari Kibajeti.