Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 65 2016-09-13

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMASI A. MAIGE aliuliza:-
Sehemu kubwa ya Jimbo la Tabora Kaskazini, Uyui halina maji chini ya ardhi na hivyo wananchi hawawezi kupata maji kwa kuchimba visima, hivyo Serikali ikabuni mradi wa kuleta maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria kupitia Shinyanga, Kahama, Nzega mpaka Isikizya na maeneo mengine ya Mkoa wa Tabora.
(a) Je, ni lini Serikali itatekeleza mradi huo ili wananchi wa Jimbo la Tabora Kaskazini katika vijiji vya Isikizya, Upuge, Majengo na Kanyenye wapate huduma ya maji?
(b) Kwa kuwa bomba hilo la maji litatoa maji umbali wa kilometa 25 kushoto na kulia na kuwafikia wananchi wachache; je, Serikali haioni kuna sababu ya kuanzisha mradi wa kuchimba mabwawa na kukinga maji ya mvua kama chanzo kingine cha maji kwa wananchi?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka katika Miji ya Tabora, Igunga, Nzega na Sikonge pamoja na vijiji 89 vilivyopo ndani ya kilometa 12 kwa kila upande kutoka bomba kuu. Kwa sasa taratibu za kupata wakandarasi wa ujenzi wa mradi huo zinaendelea ambapo ujenzi wa mradi unategemewa kuanza mwezi Disemba, mwaka huu wa 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, bomba kuu la kutoa maji Ziwa Victoria litahudumia vijiji vilivyopo ndani ya kilometa 12 kila upande. Aidha, Serikali itaendelea kubuni vyanzo vingine vya maji ikiwemo ujenzi wa mabwawa ya uvunaji maji ya mvua na uchimbaji wa visima virefu ambapo katika mwaka wa fedha 2016/2017 imetenga kiasi cha shilingi milioni 754.4 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji katika vijiji vya Halmashauri ya Uyui.