Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 76 2016-09-14

Name

Rashid Ali Abdallah

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. RASHID ALI ABDALLAH aliuliza:-
Nchi inakuwa na amani pale ambapo kuna ulinzi imara.
Je, ni utaratibu upi mzuri wa kuimarisha ulinzi Bungeni?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Ali Abdallah, Mbunge wa Tumbe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina utaratibu za kulinda maeneo yote tete kwa ustawi wa jamiii husika ikiwa ni pamoja na Bunge letu Tukufu. Kuna ulinzi wa kutumia vifaa vya kisasa na vinginevyo ambavyo ni automated, ulinzi unaoonekana na ule usioonekana ambao hufanywa na askari na ule unaofanywa na wanyama kama mbwa. Yote haya hufanyika kwa pamoja na tunakuwa na ulinzi imara katika maeneo yetu kwani huwezi kutegemea aina moja tu ya ulinzi.