Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 36 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 300 2016-06-03

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CATHERINE V. MAGIGE aliuliza:-
Mgogoro wa mipaka kati ya Hifadhi ya Serengeti na Vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro ni wa muda mrefu na sasa umekuwa sugu na kusababisha kero kwa wananchi wa maeneo hayo:-
Je, ni lini Serikali itaainisha mipaka ya maeneo hayo ili kumaliza mgogoro huu?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Catherine Valentine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na migogoro ya mipaka baina ya Hifadhi ya Serengeti na baadhi ya vijiji katika Wilaya za Serengeti, Bunda, Ngorongoro, Tarime, Busega, Bariadi na Meatu.
Kwa upande wa Wilaya ya Ngorongoro, Vijiji vinavyohusika ni pamoja na Ololosokwani, Soitsambu, Maaroni, Arashi, Piyaya, Orelian na Magaidulu. Kwa kiasi kikubwa migogoro ya mipaka katika vijiji hivi imechangiwa na kutohakikiwa kwa mipaka ya hifadhi baada ya Tangazo la Serikali Na. 235 la tarehe 21 Juni, 1968, zoezi ambalo lingefuatiwa na uwekaji wa alama za kudumu chini ya usimamizi wa kitaalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya mipaka katika Vijiji vya Wilaya za Serengeti, Bunda, Tarime, Busega, Bariadi na Meatu ilipatiwa ufumbuzi baada ya zoezi shirikishi miongoni mwa wadau wa pande za migogoro na wataalam wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, pamoja na jitihada zote zilizofanyika ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa wananchi na viongozi wa vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro ambavyo eneo lake kwa ujumla lina umuhimu mkubwa na wa kipekee kiikolojia, wananchi hawa walikataa kutoa ushirikiano na hivyo kukwamisha zoezi hilo. Wizara yangu imeorodhesha mgogoro huu wa mpaka baina ya Hifadhi ya Serengeti na Vijiji vya Wilaya ya Ngorongoro vilivyotajwa hapo juu kwenye orodha ya migogoro yote ya ardhi hususani inayohusu mipaka ya Hifadhi za Taifa na misitu inayopangwa kushughulikiwa kimkakati zaidi zaidi na Serikali hivi karibuni.