Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 37 Energy and Minerals Wizara ya Madini 311 2016-06-06

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:-
Katika Mwaka wa Fedha 2014.15 Serikali iliunganisha umeme kwenye vijiji vinne tu katika Wilaya ya Hanang; hata hivyo, Mwaka 2015/2016, Serikali iliahidi kuunganisha umeme vijiji vingine 19:-
Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi hiyo, ambayo inasubiriwa kwa hamu na wananchi wa Wilaya ya Hanang?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Michael Nagu, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi kabambe wa REA awamu ya pili katika Jimbo la Hanang umevipatia umeme vijiji saba na shule za sekondari tatu kati ya Kata 19 zilizokuwa zimeombewa umeme katika awamu ya pili. Hata hivyo, vijiji vilivyobaki Hanang, vyote alivyoomba Mheshimiwa Nagu vitapatiwa umeme kwenye REA awamu ya tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji 44 alivyoomba Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu pamoja na shule za sekondari, vituo vya afya pamoja na zahanati vinatarajiwa kupatiwa umeme kwenye REA awamu ya tatu kama alivyoomba. Kazi ya kupeleka umeme katika maeneo hayo inajumuisha ujenzi wa njia ya msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 262.4, ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 169.8, lakini pia ufungaji wa transformer 54.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi hizo, kazi nyingine itakayofanyika ni kuwaunganishia umeme wateja wa awali wapatao 11,449. Kazi ya kupeleka umeme katika Jimbo la Hanang itagharimu Shilingi bilioni 15.8.