Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 37 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 305 2016-06-06

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE (K.n.y MHE SELEMANI J. ZEDI) aliuliza:-
Ujenzi wa vyumba vya upasuaji katika vituo vya afya vya Bukene na Itobo umekamilika na kwamba vifaa vyote kwa ajili ya kutoa huduma ya upasuaji vimeshafunguliwa ikiwa ni pamoja na vifaa vya kuhifadhia damu na mashine za kufulia. Je, ni jambo gani linazuia huduma za upasuaji kuanza katika vituo hivyo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli vituo vya afya vya Itobo na Bukene vimepata vifaa vyote vinavyohitajika kwa ajili ya upasuaji ambavyo vimetolewa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachokwamisha shughuli za upasuaji kuendelea katika kituo cha afya cha Itobo ni kukosekana kwa Mtaalam wa usingizi baada ya aliyekuwepo kusimamishwa kazi kwa tuhuma za rushwa. Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri umepanga kumhamisha Mtaalam huyo kutoka sehemu nyingine ili huduma za upasuaji ziweze kuendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa kituo cha Bukene mbali na mtaalam wa usingizi, kinachokwamisha ni ukosefu wa maji ya uhakika na tayari Halmashauri inafanya marekebisho hayo. Halmashauri imetakiwa kuhakikisha upungufu huo unaondolewa mapema ili huduma hizo muhimu zianze kutolewa na kuwaondolea adha wagonjwa kufuata huduma hiyo Nzega Mjini.