Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 41 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 349 2016-06-13

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR aliuliza:-
Askari wa Wilaya ya Mkoani katika Mkoa wa Kusini Pemba wanakabiliwa na tatizo la uchache wa nyumba za kuishi na ubovu wa ofisi zao:-
Je, ni lini Serikali itawajengea Askari nyumba za kuishi na ofisi za kisasa katika kituo cha Mkoani na Kengeja – Pemba?

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI (K.n.y WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Faida Mohamed Bakar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali inatambua tatizo la uchache wa nyumba za kuishi askari na ubovu wa ofisi zao; kwa sasa Jeshi la Polisi lina mpango wa kujenga nyumba za polisi nchi nzima ambapo kwa awamu ya kwanza zitajengwa nyumba 4,136 katika mikoa 17 ikihusisha Mikoa ya Tanzania Bara pamoja Mikoa ya Unguja na Pemba.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kuboresha makazi ya askari na ofisi za polisi kwa awamu kwa kadri hali ya kiuchumi itakavyoruhusu.