Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 81 2016-02-03

Name

Rwegasira Mukasa Oscar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Kwa miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na ongezeko kubwa la matukio ya ujambazi unaohusiana na uporaji wa fedha na ni muhimu sana Watanzania wakapata ufahamu kwa takwimu kuhusu ukubwa au udogo wa tatizo hilo kuliko kupata taarifa ya tukio moja moja:-
(a) Je, ni zipi takwimu sahihi na mchanganuo wa matukio ya ujambazi unaohusiana na uporaji wa fedha ikiwa ni pamoja na vifo na majeruhi ya matukio hayo kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 Kitaifa?
(b) Je, ni mikoa gani miwili inayoongoza na mikoa gani miwili yenye matukio hayo machache?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa Biharamulo Magharibi lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, matukio ya ujambazi yanayohusisha uporaji wa fedha kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015 yalikuwa kama ifuatavyo:-
Mwaka 2013 matukio 1,266; mwaka 2014 matukio 1,127; na mwaka 2015 yalikuwa 913. Jumla ya matukio yalikuwa 3,306 yaliyosababisha jumla ya vifo vya watu 91 na majeruhi 189.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, mikoa inayoongoza kwa matukio hayo katika kipindi hicho ni Dar es Salaam iliyokuwa na matukio 733, yaliyopelekea vifo vya watu 65 na majeruhi 43. Mkoa uliofuata ulikuwa ni Mara uliokuwa na matukio 375 ya uporaji yaliyosababisha vifo 11 na majeruhi sita. Aidha, Mkoa wa Kaskazini Pemba pamoja na Kusini Unguja haukuwa na matukio ya uporaji wa fedha kabisa.