Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 35 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 286 2016-06-02

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:-
Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango umechukua muda mrefu bila kukamilika na wananchi wanaendelea kupata shida ya maji:-
Je, ni lini mradi huo utakamilika na kukabidhiwa kwa wananchi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi wa maji katika Kata ya Mtwango ulianza rasmi mwezi Juni, 2015. Mradi huo katika bajeti ya mwaka 2015/2016 ulitengewa shilingi milioni 488.8 ambapo utekelezaji wa mradi huo umefikia 60%.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukamilisha mradi huo katika Bajeti ya mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imetengewa shilingi milioni 643.5 kwa ajili ya kazi zilizobaki, ili mradi huo uanze kutoa huduma ya maji kwa wananchi.