Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 35 Works, Transport and Communication Ofisi ya Rais TAMISEMI. 285 2016-06-02

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza:-
Mheshimiwa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya M. Kikwete aliahidi kujenga barabara za Mji wa Maswa zenye urefu wa kilometa tatu ndani ya Halmashauri ya Mji Mdogo wa Maswa.
Je, ni lini barabara hizo zitaanzwa kujengwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Haroon Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne kuhusu ujenzi wa barabara kilometa tatu kwa kiwango cha lami imeanza kutekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambapo katika bajeti ya mwaka 2016/2017 zimetengwa shilingi milioni 20 kwa ajili ya kazi ya usanifu wa kina (detailed design).
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua hiyo itawezesha kujulikana kwa gharama za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Hivyo, Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami baada ya kukamilika kwa usanifu wa kina na bajeti kutengwa kwa kazi hiyo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha ahadi hii inatekelezwa pamoja na ahadi nyingine zilizotolewa na viongozi kwa manufaa ya wananchi wetu.