Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 66 2024-02-02

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa msaada wa kitaalamu kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu ili kuongeza idadi ya samaki?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeweka mipango na mikakati mbalimbali ya kuhakikisha samaki wanaendelea kuwepo na wanaongezeka katika maeneo yote ya maji, ikiwemo Bwawa la Nyumba ya Mungu. Mikakati hiyo ni pamoja na kufanya tafiti na kuimarisha ushirikishwaji wa jamii na taasisi zisizo za kiserikali katika kusimamia na kulinda rasilimali za uvuvi kupitia Halmashauri, Serikali za Vijiji na Vikundi vya kijamii vya Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi (BMU).

Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kufanya tafiti za kujua wingi na mtawanyiko wa samaki katika maziwa makuu na imejipanga kutanua wigo wa kufanya tafiti (frame survey) kwa maziwa madogo ili kutambua hali halisi ya uvuvi katika maziwa hayo. Aidha, tafiti hizo zinatoa taarifa sahihi ili kuiwezesha Wizara kutekeleza mikakati ya kuongeza wingi wa samaki ikiwemo uwezekano wa kupandikiza samaki.

Mheshimiwa Spika, napenda kulieleza Bunge lako Tukufu kuwa, Wizara itaendelea na utoaji wa elimu ya Huduma za Ugani kuhusu athari za uvuvi haramu ili kulinda mazalia ya samaki na kuruhusu samaki kukua na kuongezeka kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.