Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Madini 63 2024-02-02

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -

Je, lini Wananchi wa Nyambalembo, Magema, Katoma, Mizingamo, Katumai na Nyakabale wanaoishi eneo la leseni ya GGM watalipwa fidia?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Constantine John Kanyasu, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikishughulikia mgogoro baina ya wananchi na Mgodi wa GGM kwa kufanya majadiliano na mgodi huo ili kutafuta muafaka wa namna bora ya kumaliza migogoro katika kila eneo husika, ikiwa ni pamoja na ulipaji wa fidia stahiki. Majadiliano hayo yanaendelea katika maeneo ambayo bado hayajapatiwa utatuzi wa pamoja kuhusiana na ulipwaji wa fidia. Majadiliano yakikamilika Wizara itatoa taarifa. Kwa maeneo ambayo hayakuwa na ubishani wa upande wowote, zoezi la uthamini wa ardhi na mali za wananchi wanaoishi katika maeneo hayo, linaendelea kwa ajili ya ulipwaji wa fidia.

Mheshimiwa Spika, aidha, napenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kuwa, taratibu za uthamini wa ardhi na mali za wananchi wanaoishi katika eneo la Samina ambalo nalo liko ndani ya leseni ya GGM zinaendelea, ahsante sana.