Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 64 2024-02-02

Name

Mustafa Mwinyikondo Rajab

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dimani

Primary Question

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB aliuliza:-

Je, lini Serikali itarejesha huduma za afya zilizokuwa zikitolewa kwa wananchi na zahanati ya jeshi, Kambi ya Jeshi Kisakasaka?

Name

Dr. Stergomena Lawrence Tax

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mustafa Mwinyikondo, Mbunge wa Dimani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Kisakasaka ni Kiteule cha 672 Rejimenti ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tazania ambayo ina kikundi kidogo cha Maafisa na Askari. Kiteule hiki hutoa huduma za matibabu za msingi zinazojumuisha madawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa Wanajeshi waliopo katika Kiteule hicho. Maafisa na Askari waliopo katika Kiteule hicho wanapozidiwa hupelekwa katika Zahanati ya Kikosi Mama iliyopo maeneo ya Welezo umbali wa kilometa 17.

Mheshimiwa Spika, hapo awali Kiteule hiki kilikuwa kinatoa huduma za afya kwa Wanajeshi na wananchi, Huduma kwa wananchi zilisitishwa mwaka 2010 kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za miundombinu kutokukidhi kutoa huduma kwa wananchi wengi na upungufu wa watalaam wa tiba.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika eneo la Kisakasaka kipo Kituo cha Afya cha Fuoni Kibondeni cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kilichoanzishwa mwaka 2004, ninapenda kuwaomba wananchi waendelee kupata huduma kupitia kituo hicho wakati Wizara inatekeleza mkakati wa kuimarisha huduma za afya Jeshini, kwa kufanya maboresho katika hospitali za kanda, vituo vya afya na zahanati zilizopo katika vikosi chini ya kamandi mbalimbali nchini, zikiwemo zahanati za Jeshi zilizopo Zanzibar, ahsante.