Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 62 2024-02-02

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatatua tatizo la usafiri kwa ajili ya kusafirisha mahabusu na wafungwa katika magereza nchini?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua changamoto iliyopo ya magari ya kusafirisha mahabusu na wafungwa kwa kuwapeleka Mahakamani na kuwarudisha gerezani. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali kupitia Jeshi la Magereza ilitenga kiasi cha shilingi 878,125,000.00 katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya ununuzi wa magari matano ya kusafirishia mahabusu na wafungwa katika Magereza nchini. Aidha, katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 Serikali imetenga fedha, kiasi cha shilingi bilioni 1.93 kwa ajili ya ununuzi wa magari 14 kwa ajili ya kusafirisha mahabusu na wafungwa katika magereza nchini. Nashukuru.