Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 60 2024-02-02

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-

Je, lini Serikali itakarabati au kujenga Mahakama mpya ya Wilaya ya Ukerewe?

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mahakama inaendelea na utekelezaji wa mpango wa kujenga na kukarabati majengo katika ngazi mbalimbali. Aidha, katika ngazi ya Mahakama za Wilaya, bado tuna Wilaya ambazo hatuna majengo na hivyo, kulazimika kutumia majengo ya kuazima kwenye taasisi nyingine kama Ofisi za Wakuu wa Wilaya na Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe kwa sasa inafanya kazi kwenye majengo ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya. Hata hivyo, katika mpango wetu wa ujenzi na ukarabati wa majengo ya Mahakama, tumepanga kujenga Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe katika mwaka wa fedha 2024/2025. Naomba nitumie fursa hii kuishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kwa kutupatia kiwanja kwa ajili ya kujenga jengo hilo.