Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 56 2024-02-02

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. TARIMBA G. ABBAS aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali juu ya Bima za Afya kwa watoto?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali kuhusu Bima ya Afya kwa Watoto ni kuwaomba Watanzania wote, viongozi wote, kisiasa, kidini na kimila kuwa suluhu pekee ni sisi wote kuungana na Serikali katika kuhamasisha umma kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote pale utekelezaji utakapoanza, naomba kuwasilisha.