Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 1 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 1 2024-01-30

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: -

Je, kwa nini Baraza la kushauri masuala ya Watu Wenye Ulemavu linashindwa kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Baraza la Ushauri la Taifa la Watu wenye Ulemavu limeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya mwaka 2010 sehemu ya tatu Kifungu cha 8 hadi 12. Aidha, Sheria hiyo imefafanua majukumu ya Baraza hili ikiwa ni pamoja na kumshauri Waziri anayehusika na Watu Wenye Ulemavu juu ya utekelezaji wa Sheria za Watu wenye Ulemavu na Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 hususani katika utoaji wa haki, usawa baina ya Wanawake na Wanaume wenye Ulemavu, masuala ya afya, marekebisho, elimu, ajira, miundombinu, mafunzo ya ufundi stadi na haki nyingine kama zilivyo katika Sheria hiyo.

Mheshimiwa Spika, Baraza limekuwa likiendelea kutekeleza majukumu yake ya kuishauri Serikali kama nilivyoeleza katika aya ya kwanza.