Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Planning and Investment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 52 2024-02-02

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:-

Je, Serikali ina Mkakati gani wa kufanya utafiti maalum katika Mji wa Tunduma ili kubaini ni namna gani unaweza kuchangia kukuza uchumi wa nchi?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Mipango, hususan kifungu cha 6, pamoja na majukumu mengine, Tume ya Mipango ina jukumu la kufanya utafiti kuhusu suala lolote ambalo Tume inaona ni muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo ya Taifa. Kwa kuzingatia hili, Tume ya Mipango imejipanga kufanya tafiti mbalimbali na kuratibu tafiti zitakazofanywa na taasisi nyingine za umma na binafsi kwa lengo la kubaini fursa za maendeleo katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Spika, hivyo, Serikali, kupitia Tume ya Mipango, itafanya tafiti mbalimbali kubaini fursa za maendeleo katika miji ikiwemo Mji wa Tunduma kwa lengo kubaini ni jinsi gani mji huu na miji mingine nchini inaweza kuongeza kasi ya maendeleo na kuchangia kukuza uchumi wa nchi, ahsante.