Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 50 2024-02-02

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:-

Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Afya cha Migoli katika Jimbo la Ismani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka shilingi milioni 400 katika Halmashauri ya Iringa kwa ajili ya ujenzi wa majengo matatu ya Kituo cha Afya Migoli. Ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje umekamilika na linatoa huduma, majengo ya wodi ya wazazi na upasuaji yako asilimia 90 ya ukamilishaji.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la wazazi na upasuaji, ujenzi wa vyoo, ujenzi wa kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa awamu kwa ajili ya ujenzi, ukamilishaji na ukarabati wa miundombinu katika Kituo cha Afya cha Migoli.