Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 49 2024-02-02

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuvisaidia vikundi vya uzalishaji mali vikiwemo vya ufugaji ambavyo wanawake wamehamasika ili wafuge kwa tija?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantumu Mzamili Zodo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri za Mkoa wa Tanga na maeneo mengine nchini, zimekuwa zikitoa mikopo ya uwezeshaji kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani. Mikopo hiyo imekuwa ikitumika kwenye shughuli mbalimbali za uzalishaji ikiwemo ufugaji.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na 2022/2023, Halmashauri za Mkoa wa Tanga zilitoa mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri yenye thamani ya shilingi bilioni 4.569 ambapo kati ya fedha hizo shilingi bilioni 1.827 zilikopeshwa kwa vikundi vya wanawake ambapo vikundi 102 vya wanawake vyenye wanufaika 875 vinavyojishughulisha na kazi za ufugaji vimekopeshwa kiasi cha shilingi milioni 575.39.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuviwezesha vikundi mbalimbali kwenye shughuli za uchumi na uzalishaji ikiwemo vikundi vya akina mama ili kutengeneza ajira, kipato na hivyo kupunguza umaskini.