Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 26 2024-04-03

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali kwa Barabara ya Murushaka - Murongo ambayo Mkandarasi amepatikana zaidi ya mwaka mmoja bila Mkataba kusainiwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Seba Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkataba wa Ujenzi wa Barabara ya Murushaka – Murongo yenye urefu wa kilometa 125, sehemu ya Kyerwa – Omurushaka kilometa 50, kati ya TANROADS na Mkandarasi Shandong Company Limited umesainiwa tarehe 19 Februari, 2024. Ahsante.