Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Water and Irrigation Wizara ya Maji 23 2024-04-03

Name

Geoffrey Idelphonce Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Masasi Mjini

Primary Question

MHE. GEOFFREY I. MWAMBE aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha usanifu wa mradi wa maji ya Mto Rufiji yatokayo Bwawa la Julius Nyerere kupeleka Mikoa ya Lindi na Mtwara?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Geoffrey Idelphonce Mwambe, Mbunge wa Jimbo la Masasi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na taratibu za tathmini ya awali ya usanifu wa Mradi wa Maji wa Mto Rufiji kutoka katika Bwawa la Mwalimu Julius Nyerere, kupeleka kwenye Mikoa ya Lindi na Mtwara kwa lengo la kuhakikisha inaongeza hali ya upatikanaji wa maji katika mikoa hiyo. Aidha, Serikali inaendelea na mapitio ya usanifu wa Mradi wa Kutoa Maji katika Mto Ruvuma kwenda kwenye Mikoa ya Mtwara na Lindi na maeneo ya pembezoni yatakayopitiwa na bomba kuu.