Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 15 Sitting 2 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 19 2024-04-03

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:-

Je, kuna mpango gani wa kupandisha madaraja kwa mserereko Walimu wenye changamoto ya kupandishwa madaraja wakiwemo wa Ngara?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kifungu cha 6(a) na (3) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura 298 kikisomwa pamoja na Kanuni ya 17(5) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za Mwaka 2022; upandishaji vyeo watumishi wa umma pamoja na vigezo vingine huzingatia sifa za kielimu na kitaaluma zilizoainishwa katika miundo ya maendeleo ya utumishi, utendaji mzuri wa kazi, uwepo wa bajeti na maelekezo mbalimbali yanayotolewa na ofisi yangu kuhusu utekelezaji wa ikama na bajeti kwa mwaka husika.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia miongozo hiyo, ofisi yangu imeendelea kuhakiki taarifa na kuwapandisha vyeo watumishi wa kada ya ualimu waliobainishwa na waajiri kuwa na changamoto katika upandishwaji vyeo wakiwemo Walimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngara.

Mheshimiwa Spika, naliahidi Bunge lako kuwa, zoezi hili litakapokamilika, watumishi wa kada ya ualimu waliobainishwa na waajiri wao, wakiwemo Walimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara waliothibitishwa kuwa wametimiza sifa za kupanda madaraja watapandishwa.