Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 29 2023-11-01

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, lini elimu ya uvuvi na mikopo ya vifaa vya kisasa vitatolewa kwa wananchi wa Manda, Ruhuhu, Iwela, Lupingu, Lifuma, Makonde, Kilondo na Lumbila?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika awamu ya kwanza ya mradi wa kuwawezesha wavuvi boti za kisasa, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa jumla ya boti nne za kisasa kwa wavuvi wa Ziwa Nyasa. Kati ya boti hizo, boti mbili zimetengwa kwa wanufaika wa Halmashauri ya Ludewa ambazo nitazikabidhi kwa wanufaika hao hivi karibuni. Aidha, katika hatua za awali za upatikanaji wa wanufaika wa mikopo hiyo, wavuvi wa Ludewa Kata za Manda, Ruhuhu, Lumbila, Lupingu na Ludewa walipatiwa elimu na mafunzo ya uvuvi endelevu na utaratibu, upatikanaji na urejeshaji wa mikopo yaliyofanyika Tarehe 16 - 25 Oktoba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2023/2024, Wizara imetenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi boti za kisasa ambazo zitatolewa kwa wavuvi wa maeneo yenye shughuli za uvuvi hapa nchini ikiwemo Halmashauri ya Ludewa. Aidha, katika mwaka huu wa fedha, Wizara itaendelea kutoa elimu na mafunzo ya uvuvi endelevu, ujasiriamali katika uvuvi na namna ya kunufaika na fursa za mikopo kutoka taasisi mbalimbali za fedha ikiwemo TADB kwa wananchi wa maeneo ya uvuvi ikiwemo Ludewa. Ahsante.