Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 28 2023-11-01

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: -

Je, Serikali imefanya utafiti kuhusu uwepo wa Madini Mkoani Mtwara?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia GST imefanya utafiti wa awali na kuainisha madini yapatikanayo katika Mkoa wa Mtwara. Miongoni mwa madini hayo ni kinywe, vito aina ya ruby, sapphire, rhodolite, amazonite na green tourmaline. Pia madini ya metali aina ya dhahabu, shaba, manganese na chuma. Vilevile madini ya viwanda kama marble na chokaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, madini mengine ni mchanga wenye madini mazito (heavy minerals) kama rutile, titanium, ilmenite, zircon na magnetite, ahsante sana.