Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Finance Wizara ya Fedha 23 2023-11-01

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuweka Kituo cha Forodha Kakozi Momba ili kuunga mkono jitihada za kujenga Soko la Mazao la Kimataifa?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania ina utaratibu wa kupitia na kufanya tathmini ya sehemu zote ambazo zinaweza kujengwa ofisi kwa ajili ya ukusanyaji kodi. Utaratibu huu unazingatia uwiano wa gharama za ukusanyaji wa mapato na kiwango cha kodi kinachotarajiwa kukusanywa pindi ofisi hizo zitakapofunguliwa kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi katika eneo husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na mwenendo wa kukua kwa biashara kati ya Tanzania na nchi jirani, Serikali inaendelea kufanya tathmini ya kina katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kakozi Momba na mipaka mbalimbali hapa nchini. Aidha, maeneo yatakayokidhi vigezo vya kujengwa ofisi za forodha kulingana na tathmini hiyo, taratibu za uanzishwaji wa ofisi hizo zitaanza kwa kuzingatia upatikanaji wa rasilimali watu na fedha. Ahsante.