Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 21 2023-11-01

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATAUS P. MWANYIKA aliuliza: -

Je, kwa nini Sheria za Ardhi zinazokusudiwa kutumika kwenye miji zinatumika maeneo ya vijijini?

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mfumo wa kisheria wa usimamizi wa ardhi nchini umegawa ardhi katika makundi matatu ambayo ni Ardhi ya Kijiji, Ardhi ya Hifadhi na Ardhi ya Jumla. Kwa kuzingatia mgawanyo huo, Ardhi ya Vijiji inasimamiwa na Sheria ya Ardhi ya Vijiji, Sura 114 na maeneo ya miji yanasimamiwa na Sheria ya Ardhi, Sura 113. Hata hivyo, yapo baadhi ya maeneo ndani ya mipaka ya vijiji yanayosimamiwa na Sheria ya Ardhi, Sura 113 kutokana na kumilikishwa kabla ya kuanza kutumika kwa Sheria ya Ardhi ya Vijiji, Sura 114 au kuhawilishwa. Aidha, baadhi ya maeneo ya vijiji yametangazwa kuwa ya kuendelezwa kimji (Planning Area) na kuandaliwa Mpango Kabambe (Master Plan) na hivyo kuyafanya yasimamiwe na Sheria ya Ardhi, Sura 113.