Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 3 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 42 2024-02-01

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI aliuliza: -

Je, sababu zipi zinasababisha eneo linaloathiriwa na mabadiliko ya tabianchi kupewa kipaumbele cha utekelezaji wa Mradi ili kunusuru hali hiyo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simai Hassan Sadiki, Mbunge wa Jimbo la Nungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mabadiliko ya tabianchi yanazidi kusababisha athari katika maeneo mbalimbali ya nchini yakiwemo maeneo ya ukanda wa pwani nchini. Katika kubainisha maeneo yaliyoathirika na kuyaweka katika kipaumbele, Serikali inafanya tathmini ya kiwango cha uharibifu na athari zilizojitokeza hii ni moja ya sababu mojawapo ya vigezo vinavyotumika katika kuweka kipaumbele maeneo yaliyoathirika katika mipango ya utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itaendelea kubaini maeneo mbalimbali yenye changamoto kubwa ya uharibifu wa Mazingira na kuyaweka katika kipaumbele ili kuyatafutia rasilimali fedha, nashukuru.