Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Investment and Empowerment Ofisi ya Rais: Mipango na Uwekezaji 13 2023-11-01

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua na kutangaza maeneo ya uwekezaji Mkoani Kigoma?

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

NAIBU WA VIWANDA NA BIASHARA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kavejuru Eliadory Felix, Mbunge wa Buhigwe kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkakati wa Serikali ni kuendelea kuzitangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini zikiwemo zinazopatikana Mkoani Kigoma. Miongoni mwa mikakati hiyo ni kuandaa makala maalum (documentary) ya kutangaza maeneo ya uwekezaji katika Mkoa wa Kigoma, pia, kufanya makongamano ya kimataifa ya biashara na uwekezaji, ambapo kongamano la kwanza lilifanyika mwaka 2019 na la pili lilifanyika mwaka 2022. Aidha, mwezi Mei, 2024, Mkoa wa Kigoma unatarajia kufanya Kongamano la tatu la Kimataifa la Biashara na Uwekezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutangaza maeneo ya uwekezaji kupitia ziara za viongozi wa Kitaifa ndani na nje ya nchi na kupitia ofisi zetu za balozi zetu, nakushukuru sana.