Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2023-11-01

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuhakikisha upatikanaji wa vifaa kwa maabara ya sayansi katika shule za Mkoa wa Katavi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Festo Mariki, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia mpango wa kuboresha elimu ya sekondari katika mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga shilingi bilioni 5.148 kwa ajili ya kununua vifaa vya maabara ili viweze kusambazwa katika shule za sekondari kote nchini ikiwemo shule za Mkoa wa Katavi. Ununuzi wa vifaa hivyo upo katika hatua za mwisho kulingana na taratibu za manunuzi.

Aidha, katika Mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali ilipeleka vifaa vya Maabara katika Shule za Mbede, Usevya, Mizengo Pinda, Mamba, Chamalendi, Kasansa, Kabungu, Karema, Mpandandogo, Kandamilumba, Mwese, Kapalamsenga na Homera zilizopo kwenye Mkoa wa Katavi.