Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 2 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 9 2023-11-01

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. CHARLES J. MWIJAGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka Fibre Speed Boat mbili zilizofunikwa kama ambulance ili kusaidia Wananchi wa Visiwa 39 vya Wilaya ya Muleba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mhe Charles John Mwijage, Mbunge wa Jimbo la Muleba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kwa kushirikiana na Wizara ya Afya imeandaa mpango mkakati utakaowezesha maeneo magumu kufikika kama visiwani na maeneo mengine kupata huduma za usafiri wa dharura pindi utakapohitajika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huo umeainisha vifaa vya usafiri vitakavyotumika kusafirisha wagonjwa ikiwemo usafiri wa anga yaani air ambulance na usafiri wa maji yani boat ambulance. Aidha, Mpango huo unatarajiwa kukamilika Disemba 2023 na kuanza utekelezaji katika mwaka wa fedha 2024/2025 na Wilaya ya Muleba itapewa kipaumbele, ahsante.