Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 125 2024-02-07

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwa wananchi wanaoishi kwenye mitaa 17 ya Mamlaka ya Mji Mdogo Rulenge – Ngara?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ndaisaba George Ruhoro, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza miradi mbalimbali ya kupeleka umeme kwenye vijiji na vitongoji ambapo kupitia mradi wa REA awamu ya Tatu mzunguko wa pili, vijiji 32 vya Wilaya ya Ngara vitapata umeme. Aidha, Wakala wa Nishati Vijijini yupo katika hatua za mwisho za kukamilisha taratibu za ununuzi wa kuwapata wakandarasi wa kutekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye vitongoji (Hamlet Electrification Project - HEP), ambapo vitongoji 15 katika Jimbo la Ngara vitapatiwa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa mitaa 17 katika Mamlaka ya Mji mdogo wa Rulenge, Serikali kupitia TANESCO na REA itatenga bajeti katika mwaka ujao wa fedha ili kuwapatia umeme wananchi wanaoishi katika maeneo hayo.