Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 120 2024-02-07

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. MRISHO M. GAMBO aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kuunganisha mita za maji za kulipia kabla ya matumizi kama za TANESCO Arusha Mjini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Arusha (AWSA) imeshaanza kufunga dira za malipo ya kabla kwa taasisi za Serikali na baadhi ya wateja wa kawaida. Mpaka sasa jumla dira 345 zimeshafungwa na zoezi la ufungaji wa dira hizo linaendelea. Baadhi ya Taasisi za Serikali zilizofungwa dira hizo ni pamoja na Jeshi la Polisi, ofisi pamoja na nyumba za watumishi, ofisi za Serikali, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Ofisi ya NIDA, Ofisi za Kata, Ofisi za Magereza na Makumbusho, baadhi ya vituo vya afya na zahanati pamoja na Shule za Msingi na Sekondari zimeshafungiwa dira hizo.