Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
1961-1995 Session 1 Sitting 1 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 117 2024-02-07

Name

Antipas Zeno Mngungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, mchakato wa kuwa na Vazi la Taifa umefikia hatua gani?

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo iliunda Kamati ya Kitaifa ya kuratibu upatikanaji wa Vazi la Taifa. Kamati hiyo imefanikiwa kukusanya maoni kutoka kwa wadau na wananchi 2,452 kutoka Mikoa yote Tanzania Bara na Visiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua iliyofikiwa kwa sasa ni kuwa, Kamati itakutana ili kuwashindanisha wabunifu wa mavazi (designers), kutoka pande zote mbili za Muungano ili wale watakaokuwa washindi kwa upande wa wanaume na wanawake mavazi yao ndiyo yatakayopendekezwa kuwa vazi la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wabunifu hao watafanya kazi kwa kutumia maoni na mapendekezo yaliyotolewa na wadau pamoja na wananchi ili kukamilisha mchakato wa upatikanaji wa vazi la Taifa kwa ufanisi na haraka zaidi. Aidha, tumeamua kutumia njia hii ili kuharakisha mchakato na kupunguza uhitaji wa matumizi ya fedha nyingi za uratibu wa upatikanaji wa vazi la Taifa. Ahsante.