Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 110 2024-02-07

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Ngerengere kilisajiliwa mwezi Mei, 1995 na kinatoa huduma ya ngazi ya Kituo cha Afya ikiwa ni pamoja na huduma za upasuaji wa dharura na huduma nyingine. Aidha, kituo hiki kinahudumia wastani wa wagonjwa 1,200 kwa mwezi na 14,000 kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hiki kina upungufu wa baadhi ya miundombinu ikiwemo jengo la Huduma za Mama na Mtoto na Upasuaji, jengo la Maabara, jengo la kuhifadhia maiti na jengo la kufulia. Eneo la Kituo hicho lina ukubwa wa ekari nne na nusu, hivyo halitoshelezi mahitaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, inaendelea kufanya mazungumzo na Shirika la Posta ambalo linamiliki eneo mkabala lenye ukubwa wa ekari mbili ambalo halijaendelezwa ili litumike kupanua Kituo cha Afya cha Ngerengere, ahsante.