Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2024-02-07

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:-

Je, lini Serikali itatimiza ahadi ya kupeleka majokofu manne ya mochwari kwenye Kituo cha Afya Mugeta?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha upatikanaji wa vifaatiba ikiwemo majokofu ya kuhifadhia maiti katika vituo vya huduma za afya. Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali ilitenga na kupeleka shilingi milioni 700 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwa Halmashauri ya Bunda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi milioni 32.7 kimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa jokofu moja la milango sita la Kituo cha Afya cha Mugeta. Taratibu za manunuzi zinafanyika kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) na inatarajiwa kukamilika kati ya mwezi huu Februari na Machi 2024. Ahsante.