Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Water and Irrigation Wizara ya Maji 187 2024-02-13

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha uchimbaji wa visima vya maji vilivyoanza kuchimbwa katika Jimbo la Buchosa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer


NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Jimbo la Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa 2023/2024 Serikali inaendelea na zoezi la utafiti wa maji chini ya ardhi pamoja na uchimbaji wa visima 13 katika Jimbo la Buchosa Wilayani Sengerema. Hadi sasa jumla ya visima sita vimechimbwa, ambapo kati ya visima hivyo tulivyopata maji ni visima vinne vilivyochimbwa katika vijiji vya Bulolo, Nyonga, Bulyahilu na Izindabo. Aidha, kazi ya utafiti wa maji ardhini na uchimbaji wa visima inaendelea katika Vijiji vya Kisaba, Busikimbi, Kasalaji, Nyamiswi, Luharanyonga, Irenza na Bugoro ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2024.