Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Community Development, Gender and Children Wizari wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto 185 2024-02-13

Name

Janeth Elias Mahawanga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANETH E. MAHAWANGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza tatizo la mimba za utotoni kwa watoto wa kike?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Janeth Elias Mahawanga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kushirikiana na wadau, imekuwa ikitekeleza afua mbalimbali kupitia Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA). Ambapo Serikali inatarajia kuzindua Awamu ya Pili ya Mpango Kazi huo mwezi Machi, 2024; ambapo moja ya kipaumbele chake ni mikakati ya kudhibiti mimba za utotoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na afua zinazotekelezwa katika mpango huo Serikali itaendelea kutekeleza afua mambo yafuatayo: -

(i) Kufanya kazi kwa mapitio ya Sheria ya Elimu ya mwaka 1978 ambayo imeongeza adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa atakayepatikana na hatia ya kumpa mimba mtoto/mwanafunzi shule/.

(ii) Kuendelea kutoa elimu ya stadi za maisha kwa watoto kupitia madawati ya ulinzi na usalama wa mtoto na kutoa elimu ya malezi na makuzi ya watoto kwa wazazi au walezi na jamii kupitia kampeni katika vyombo vya habari na majukwaa ya madhehebu ya dini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali imepanga kuzindua Kampeni ya Usalama wa Mtoto Mtandaoni kwa ajili ya kuelimisha wazazi, walimu na watoto kuhusu athari za matumizi yasiyofaa ya mitandao ambayo pia yanachangia mimba za utotoni.