Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 183 2024-02-13

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati ghala la mazao lililopo katika kata ya Ludewa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Jimbo la Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara inatambua umuhimu wa ghala la Ludewa katika kuwezesha soko la mahindi kwa wakulima wa Kata ya Ludewa. Ghala hilo lilikuwa kituo muhimu cha ununuzi wa mahindi kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) lakini kwa sasa halitumiki kwa kuwa limechakaa na kupata nyufa kubwa kiasi cha kutokidhi vigezo vya uhifadhi mazao ya kilimo. Aidha, uwezo wa ghala hilo ni mdogo (tani 150) ikilinganishwa na uzalishaji wa mahindi katika Kata hiyo ambao ni takriban tani 27,000 kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia changamoto hiyo, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kwa kushirikiana na uongozi wa kata hiyo tayari imeainisha eneo lenye ukubwa wa ekari 4 kwa ajili ya ujenzi wa ghala lenye uwezo wa kuhifadhi tani 2,000. Aidha, michoro na makadirio ya mahitaji ya ujenzi (BoQ) vimeandaliwa na hivyo ghala hilo litaingizwa kwenye mpango wa ujenzi kulingana na upatikanaji wa fedha.