Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 84 2023-11-06

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:-

Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa ardhi kati ya mwekezaji wa Shamba la Malonje na wananchi wa Kata ya Muungano na Mollo Kwela?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dues Clement Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Shamba la Malonje linalojulikana kama Shamba Namba 48/1 Malonje katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na Manispaa ya Sumbawanga lenye ukubwa wa hekta 10,002 liliuzwa na Serikali kwa mwekezaji ambaye pia ni Bodi ya Wadhamini wa Efatha Ministry. Mgogoro wa ardhi katika shamba hili unasababishwa na baadhi ya wananchi kutoka katika vijiji vya Msanda Muungano, Sikaungu na Songambele Azimio katika maeneo ya shamba hili yaliyo ndani ya mipaka kutwaliwa kinyume cha utaratibu.

Mheshimiwa Spika, katika kushughulikia suala hili, Serikali iliwasilisha maombi kwa mwekezaji kumega sehemu ya shamba ili igawiwe kwa wananchi na vijiji vinavyozunguka shamba hilo kwa ajili ya shughuli za kilimo. Pamoja na mwekezaji kuridhia kumega sehemu ya shamba lenye ukubwa wa ekari 3,000 ili angalau kila kijiji kipate ekari 1,000 bado wananchi wameendelea kuvamia shamba la mwekezaji.

Mheshimiwa Spika, natoa rai kwa uongozi wa Mkoa na Wilaya kusimamia upangaji na ugawaji wa ardhi iliyotolewa na mwekezaji kwa vijiji hivyo ili kuondoa mgogoro uliopo. Aidha, uongozi wa Mkoa na Wilaya uwaelimishe wananchi juu ya kuheshimu mipaka ya ardhi ya mwekezaji kwa kuwa anamiliki eneo hilo kisheria.