Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 75 2023-11-06

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuongeza bei ya chai Wilayani Rungwe kutoka shilingi 340 hadi shilingi 700 kwa kilo hasa ikizingatiwa kupanda kwa gharama za mbolea na madawa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha mkulima wa chai anapata bei nzuri Serikali kwa kushirikiana na Sekta Binafsi imedhamiria kuanzisha mnada wa chai nchini ili kupunguza gharama za usafirishaji na uhifadhi wa chai kwenye maghala katika mnada wa Mombasa. Mnada utasaidia upatikanaji wa soko la uhakika kwa wakulima na kuimarisha bei ya chai nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia itaendelea kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya kuchanganya na kufunga chai nchini ili kupunguza utegemezi wa soko la nje. Hatua hii itaendelea kupanua soko la ndani na kuimarisha bei ya chai nchini.