Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 13 Sitting 6 Good Governance Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 72 2023-11-06

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:-

Je, kwa nini Serikali imewaacha wananchi wengi wenye sifa na vigezo vya kunufaika na TASAF katika Jimbo la Mwibara?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Muguta Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mwibara lipo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na lina jumla ya walengwa 5,320 ambao walipatikana kwa mujibu wa taratibu zinazotumika kuwapata Walengwa. Taratibu hizi zinatoa nafasi kupitia Mkutano Mkuu wa Kijiji au Mtaa au Shehia ambapo wananchi wenyewe wanapata nafasi kupendekeza, kuchuja na kuamua juu ya nani wawepo kwenye mpango kwa mujibu wa Mwongozo wa Utambuzi wa Wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Toleo la mwaka 2019 na marejeo yake ya mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, iwapo bado kuna wananchi walipendekezwa kuwa wanufaika ila hawakuingia kwenye mpango, wawasilishe rufaa kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na rufaa hizo zitaletwa kwenye Ofisi za TASAF Makao Makuu kwa ajili ya mapitio.