Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Uchukuzi 59 2023-11-03

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Primary Question

MHE. PROF. PALAMAGAMBA J. A. M. KABUDI aliuliza: -

Je, lini Serikali itakarabati na kufufua reli kutoka Kilosa hadi Kidatu?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi, Mbunge wa Kilosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa vipindi tofauti imeendelea kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji katika maeneo mbalimbali nchini. Kuhusu ufufuaji wa reli kutoka Kilosa hadi Kidatu, Serikali kupitia TRC katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 imetenga jumla ya shilingi bilioni 3.4 kwa ajili ya kuanza kazi za awali za marekebisho na ufufuaji wa njia katika kipande hiki chenye urefu wa kilomita 108 ambayo imefungwa kwa muda mrefu zaidi. Reli hii inaunganisha Reli ya Kati na TAZARA eneo la Kidatu. Aidha, kwa sasa TRC imekamilisha tathmini ya kihandisi ikiwemo makadirio ya gharama ya mradi (Engineering estimates) na inaendelea na ukamilishaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya kumwajiri Mkandarasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutumia fursa hii kumuomba Mheshimwa Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi - Mbunge, pamoja na wananchi wa Kilosa kuwa na subira wakati Serikali inaendelea na juhudi ya urejeshwaji wa njia hii ambayo ni muhimu kwa ajili ya usafirishaji wa mizigo na abiria. Lengo la Serikali ni kuendelea kufanya maboresho katika maeneo yenye mahitaji ili wananchi waweze kuendelea kupata huduma za usafiri na usafirishaji.