Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 4 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 54 2023-11-03

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza:-

Je, ni lini TANROADS watalipa fidia kwa kujenga shule mbadala baada ya shule ya Msingi Unkuku kupitiwa na Barabara ya Dodoma – Arusha?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Dodoma ilikwishalipa fidia kwa jengo la Shule ya Msingi Unkuku, miti pamoja na sehemu ya eneo la shule ambavyo viliathiriwa na ujenzi wa barabara ya Dodoma – Babati ambapo mnamo tarehe 10 Septemba, 2014 kiasi cha shilingi 8,370,221.00 kililipwa kwa Mkurugenzi wa Halmasauri ya Wilaya ya Kondoa, ahsante.