Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 14 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 179 2024-02-13

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: -

Je, lini Serikali itatenga fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kijiji cha Magungu – Kiteto?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edward Olelekaita Kisua, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Polisi cha Magungu Kiteto ulianza mwaka 2015 kwa kutumia michango na nguvu za wananchi. Ujenzi huo ulisimama ukiwa kwenye hatua ya lenta kutokana na kukosa fedha. Wakati ujenzi unasimama kiasi cha shilingi 20,000,000 zilikuwa zimetumika. Tathmini ya kumaliza ili kuunga mkono nguvu za wananchi imeshafanyika na kiasi cha fedha shilingi 33,985,000 kinahitajika. Fedha hizo zitatengwa kwenye mfuko wa Tuzo na Tozo kwa mwaka wa fedha 2024/2025, ahsante.